TETESI ZA SOKA ULAYA

=Mshambulizi wa zamani wa Arsenal Thierry Henry anasema angependa kuchukua nafasi yake Arsene Wenger kama meneja wa Arsenal (Sky Sports).

= Chelsea ndio wako kifua mbele katika kumsaini mshambuliaji wa Bayern Munich Robert Lewandowski.
Mchezaji huyo raia wa Poland anataka kujiunga na Premier League. (Sun).

= AC Milan wana mpango wa kumsaini kiungo wa kati wa Swansea raia wa Korea Kusini Ki Sung-yueng, 29. (Calciomercato - in Italian) .

=Arsenal wanamtaka kiungo wa kati wa Paris St-Germain, Yacine Adli 27.

=Manchester City, Barcelona na Juventus pia wanamwinda raia huyo wa Ufaransa. (L'Equipe, via Sun).

= Washambuliaji wa Barcelona Lionel Messi, Luis Suarez na Philippe Coutinho wameidhinisha mipango ya klabu hiyo kuwaleta wachezaji watatu wapya msimu unaokuja. (Diario Gol - in Spanish) .

=Tottenham wanapanga kumsaini mshambulizi wa Sheffield United wa umri wa miaka 20 David Brooks. Klabu hiyo ya Premier League ina mpango wa kukubaliana pauni milioni 10 wa raia huyo wa Wales. (Sun).

= Kiungo wa kati wa Roma Radja Nainggolan alioneka kupoteza jino alipogongana na Franck Kessie wakati Roma ilishindwa na AC Milan siku ya Jumapili. (Football Italia).

= Mshambualiaji wa Paris St-Germain na Brazil Neymar, 26, amewaambia Real Madrid kuwa anataka pesa zaidi kuliko za mshambuliaji mreno Cristiano Ronaldo ili aweze kuhamia Bernabeu. (Sunday Express) .

=Kiungo wa kati mfaransa Paul Pogba yuko tayari kuondoka Manchester United ikiwa meneja Jose Mourinho ataendelea kuwepo Old Trafford. (Sun on Sunday) .

=Manchester United ni kati ya vilabu vikuu vinavyomtazana kiungo wa kati wa Lazio raia wa Serbia, Sergej Milinkovic-Savic, ambaye ambaye thamani yake huenda ikawa pauni mioni 80. (Sunday Mirror) .

=Meneja wa zamani wa Manchester United Louis van Gaal, huenda akachukua mahala pake Antonio Conte, huko Chelsea ikiwa uhusiao wake na Chlesea utazorota zaidi. (Sunday Mirror) Kwa hisani ya BBC.

posted from Bloggeroid

ASLAY, NANDY WATOZWA FAINI YA TSH MILLION 5

Wasanii wa muziki wa Bongo fleva nchini, Aslay na Nandy wamepigwa faini ya milioni 5 kwa kosa la kuimba wimbo wa Subalkheri bila kibali maalumu kutoka kwa watunzi na wamiliki wa wimbo huo ambao ni kikundi cha Utamaduni cha taarab asilia visiwani Zanzibar.

Kikundi hicho kilikusudia kuwafikisha mahakamani wasanii hao lakini kabla ya kuchukua hatu hiyo kiongozi wa Aslay na Nandy walifika visiwani humo na kufanya mazungumzo na kikundi hicho.

Ambapo viongozi hao walikiri kufanya kosa hilo la kukariri na kuimba wimbo huo bila kibali toka kwa wamiliki hao na kupitia kosa hilo kikundi hiko cha taarabu kimewataka walipwe milioni tano kama adhabu.

Katibu Mkuu wa kikundi cha utamaduni cha tarabu asilia, Taimur Rukuni Twaha, amesema kikundi hicho cha tarab kimewataka wasanii hao kulipa faini kutokana na kuimba wimbo huo bila ya ridhaaT.waha amesema licha ya kukiri makosa hayo pia meneja wa Aslay ameomba kuingia mkataba na kikundi hicho cha tarab kufanya biashara ya kuziimba tena nyimbo zao nyingine za zamani.

Katibu huyo amesema kuhusu nyimbo zao kuimbwa tena hilo bado hawajaafikiana kwa sababu walishapewa agizo na Rais mstaafu wa awamu ya tatu Dk Salmin Amour Juma wakati akiwa rais, kuwa wasikubali nyimbo zao za tarabu asilia kuzibadili na kuzifanya katika mfumo wa muziki wa kisasa.

posted from Bloggeroid