Magazeti ya Tanzania leo Januari 31, 2018



Fahamu yote yaliyojiri katika Magazeti ya Tanzania leo Januari 31 2018. Hapa unapata habari zote zilizopewa uzito katika kurasa za mbele.



posted from Bloggeroid

SHULE KUMI BORA NA SHULE KUMI ZA MWISHO KITAIFA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2017.

Katika matokeo hayo ya kidato cha nne, pamoja na kuwepo kwa upandaji wa ufaulu kwa asilimia 7, zipo shule zilizofanya vizuri zaidi kuliko nyingine na zile zilizofanya vibaya. Zifuatazo ni orodha ya shule 10, zilizofanya vizuri na zile zilizofanya vibaya.

Shule kumi (10) Bora kitaifa .

1. St. Francis Girls – Mbeya

2. Feza Boys – Dar es Salaam

3. Kemoboya – Kagera

4. Bethel Sabs Girls – Iringa

5. Anwarite Girls – Kilimanjaro

6. Marian Girls – Pwani

7. Canossa – Dar es salaam

8. Feza Girls – Dar es salaam

9. Marian Boys – Pwani

10. Shamsiye Boys – Dar es salaam


Shule Kumi (10) za Mwisho Kitaifa

1. Kusini – Kusini Unguja

2. Pwani Mchangani – Kaskazini Unguja

3. Mwenge SMZ – Mjini Magharibi

4. Langoni – Mjini Magharibi

5. Furaha – Dar es salaam

6. Mbesa – Ruvuma

7. Kabugaro – Kagera

8. Chokocho- Kusini Pemba

9. Nyeburu – Dar es salaam

10. Mtule – Kusini Unguja.
posted from Bloggeroid

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2017

Baraza la Mitihani Tanzania, limetangaza matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) na ule wa Maarifa (QT) leo juma nne 30,01,2018. Jijini Dar es salam .




Akitangaza matokeo hayo katibu Mtendaji wa Necta, Dk Charles Msonde ,amesema kuwa ufaulu wa wanafunzi kwa mwaka huu umeongezeka kwa asilimia 7 ukilinganisha na matokeo ya mwaka jana.

“Jumla ya Watahiniwa 287,713 ambao sawa na asilimia 77.09%  kwa shule za kawaida na vituo vya kujitegemea wamefaulu ambao katika ya hao wasichana wapo 143,728 sawa na asilimia 75.21% wakati wavulana wapo 143,985 sawa na asilimia 79.06%. Mwaka jana wanafunzi waliofaulu mitihani ya kidato cha nne walikuwa 277,283 ambao ni asilimia 70.09% hivyo ufaulu wa jumla umeongezeka kwa asilimia"amesema MsondeBaraza la Mitihani Tanzania, limetangaza matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) na ule wa Maarifa (QT) leo juma nne 30,01,2018. Jijini Dar es salaam.
 
             KUYAONA MATOKEO HAYO BOFYA HAPA

.
Mbali na hilo Msonde aliweza kuweka wazi kuwa jumla ya wanafunzi 265 wamebainika kufanya udanganyifu mbalimbali katika mitihani hiyo ambayo ilianza kufanyika Oktoba 30, 2016 mpaka Novemba 17, 2016 .



Endelea kutembelea blog hii tuzidi kukujuza mengi yaliyojili, ndani na nje ya nchi.
By blogger Peter Lugendo
posted from Bloggeroid