ELIMU

Uhali gani ndugu msomaji wa makala hii, ni matumaini yangu uumzima Wa afya tele. Karibu kwenye somo la leo ,kuhusu namna unavyo weza kuzitumia FURSA zisizo hitaji mtaji mkubwa kujikwamua kimaisha..
Katika hali ya kawaida kila mwanadamu anacho kitu anachoweza kukifanya Kwa ufanisi mzuri zaidi lakini hushindwa kuyafanya kutokana na sababu mbali mbali,kama vile kutojiamini, kushindwa kujitambua vizuri, hofu ya kushindwa, au kukosa MTAJI ili kufanikisha jambo hilo . Katika mambo yote hayo tatizo LA kukosa mtaji ndiyo tatizo linalo wasumbua watu wengi. Kwa kulijua hilo blog yako ya lufametz ,wameamua kukuonesha fursa 12 ambazo unaweza kujihusisha nazo Kwa kutumia mtaji mdogo sana na kujikwamua kimaisha...**

(1).KUUZA NGUO ZA MITUMBA
fursa hii haina ulazima wa kuanza Kwa mtaji mkubwa sana ,kwani unaweza kuanza na mtaji wa hata Tsh 15000/= Mfano yapo masoko kama vile tandare,karume ,mbagala na masoko mengine mikoani ambayo huuza nguo kwa bei ya chini sana ,kuanzia tsh 500/= mpaka tsh 1000/= ambazo wewe unaweza kuzinunua na kuzipeleka sehemu nyingine ambako utaweza kuziuza kuanzia 1500/= mpaka 2000/= nakukufanya ujikwamue kidogo kidogo huku ukiplan jambo kubwa zaidi..

(2).KUUZA MAYAI
[image_1] si lazima uuze wewe kama unahisi huwezi,na unaweza kuanza Kwa mtaji mdogo tu wa tray hata mbili(2) ukampa mtu akuuzie Kwa bei ya @500/= ..utaweza kuingiza tsh 12000/= Kwa tray moja, ukamlipa 2500/= aliyekuuzia ikabaki tsh 9500/= na jumla ya faida ikawa tsh 4500 mpk 4000 Kwa kila tray...Kwa namna hiyo utaweza kuongeza tray la tatu nakubakiwa na tsh 3000/= mkonon huku mtaji ukizidi kukua,hata kukuwezesha kufanya jambo jingine.

(3).KUUZA MIHOGO,VIAZI,MAHINDI N.K
Hasa yakukaanga na mahindi huweza kuwa yakuchoma au kuchemsha. Tatizo la vijana wengi hujiangalia zaidi katika hali ya ubishoo na usister duu ,hivyo kujikuta wanachagua fursa za kuanza nazo mwisho wake wanalalama kuwa hakuna fursa ..Biashara hii huweza kuanza Kwa mtaji mdogo tu wa tsh 10000/= au 15000/= nakukulipa vizuri kwani hizo ni bidhaa chakula ambazo ni lazima zitumike kila siku...

(4).KUUZA VINYWAJI VYA JUMLA
Unaweza ukahofia kuwa utahitaji kuwa na mtaji mkubwa sana ,ila hapana ,unaweza kuanza Kwa katon au kreti tano tu za soda ,na zitakapoisha utaweza kuongeza katon moja ...Na Kwa namna hiyo msingi wako utazidi kukua siku hadi siku nakufikia malengo...

(5).KUFUNDISHA TUISHENI
kama wewe ni kijana mwenye elimu inayotosha kufundisha wengine ,unaweza kujishughulisha na kufundisha Kwa kuwatoza pesa unao wafundisha na ikawa ni fursa pia kukufikisha kwenye malengo makubwa zaidi..

(6).KUANZISHA KIKUNDI AU KAMPUNI YA UZOAJI TAKA.
fursa hii inalipa kwasababu .kwanza haina watu wengi wanayojihusisha nayo. Pili taka ni vitu vinavyokuwepo Kwa wingi sana hasa kutokana na shughuli mbali mbali za kibinaadam .sio lazima ufanye wewe unaweza kuwa kama organiser au mmiliki wa kampuni hiyo na ukafanikiwa.

(7).KUUZA MAGAZETI
Fursa hii huenda ikawa rahisi zaidi kwani unaweza kuanza hata Kwa kukopeshwa magazeti.kisha ukawa unalipa baada ya kumaliza au jioni kufika.unaweza kuuza Kwa kutembeza au kuweka sehemu moja,na bado ikakulipa hata kukuwezesha kufikia malengo yako.

(8).KUFUNGUA SEHEMU YA KUFANYISHA WATU MAZOEZI
Sio lazima uanze kwa mtaji mkubwa wa vifaa kamili vya mazoezi yaani (gym). Hapana unaweza kuanza Kwa kuandaa sehemu tu na vyombo vya mziki ,pamoja na mtu aliyevizuri katika swala zima la mazoezi.ukaongeza na ubunifu wako kwani msingi mkubwa hapo ni ubunifu na ushawishi.

(9).KUANZISHA KAMPUNI YA KUCHORA MABANGO,KU design BLOGS, WEBSITES, LOGOS NA MICHORO YA MAJENGO
unachotakiwa kufanya hapa nikuwatafuta watu wenye fani hizo na kuongea nao juu ya hilo. Hutokosa watu wakufanya nao kwasababu kuna idadi kubwa ya watu wasio na ajira..kisha unatakiwa uwe bize kuitangaza kampuni yako mitandaoni ili ijulikane na watu wengi zaidi na kuongeza wateja..

(10).KUWA DALALI
Unachopaswa kuwa nacho hapa ni uaminifu,lugha nzuri Kwa watu wote,umakini na uchangamfu katika kusaka wateja.Mfano unaweza kuwa dalali kwa njia ya uuzaji wa bidhaa kwa makubaliano ya mitandaoni, ukawa unalipwa kila unapokamilisha dili.

(11).KUTOA USHAURI WA KITAALAMU
Kama wewe ni mtu mwenye ujuzi maalumi juu ya jambo fulani, unaweza kuanzisha sehemu maalum kwaajiri ya kutoa ushaur wa kitaalam juu ya swala hilo...Mfano waliosoma maswala ya IT ni rahisi zaidi kupata wateja kwani matumizi ya vifaa vya kiteknolojia yako juu sana siku hizi,na wengi wa watumiaji hawana elimu yakutosha juu ya vifaa hivyo ,Kwa mantiki hiyo hii nayo ni fursa..

(12).KUUZA UBUYU NA BIDHAA NYINGINE NDOGO NDOGO.
Kama vile karanga na ice cream na biscuits.. Biashara hizi hulipa sana .Mfano mfuko mmoja wa ubuyu unaweza kuununua Kwa tsh 1500/= mpaka 2000/= na unaweza kufunga vipakti vya 6500 au 5500/= ukiangalia hapo bado utaweza kuingiza faida itakayo kuwezesha kufikia malengo yako.

N.B: kabla yakuanza jambo lolote kati ya hayo hakikisha una taarifa kamili zifuatazo ;a) bidhaa husika zinapatikanaje? .b).soko lake likoje..c)wapi kuliko na wahitaji zaidi...d).vitu gani au watu gani wa muhimu unapaswa kuwa navyo kabla ya kuanzisha lolote...e).unaweza kuanzisha jambo Kwa kuwaweka watu pamoja kwa maelewano ya malipo ya baada ya kazi....f).utambue unataka nini ili iwe nini na kwa wakati gani...g).mwisho kabisa iandae nafsi yako vizuri kukubaliana na lolote litakalo jitokeza katika biashara yako..usiogope kukosea ila jifunze zaidi.

Hongera kwa kukubali kujifunza elimu hii ndogo ya Ujasiriamali na utambuzi wa fursa........

IMEANDALIWA NA
Lufame TZ
Karibu tena kwa makala nzuri zaidi

No comments:

Post a Comment