SIFA KUMI (10) ZA MSINGI ZA KUKUFANYA UPATE MKOPO WA ELIMU YA JUU (2017/2018)

JE, UTAOMBA MKOPO WA ELIMU YA JUU MWAKA HUU?
• ZIFUATAZO NI SIFA KUMI (10) ZA MSINGI
1. Mwombaji awe Mtanzania.
2. Mwombaji awe ameomba kudahiliwa na Chuo Kikuu au Taasisi ya Elimu
ya Juu inayotambuliwa na Serikali.
3. Asiwe mwanafunzi wa masomo ya jioni (Part time Student).
4. Asiwe na udhamini/ufadhili/msaada wa kifedha kutoka katika vyanzo
vingine.
5. Awe ameomba mkopo kupitia mfumo wa mtandao (OLAMS).
6. Awe amefaulu mitihani ya mwisho wa mwaka (wanaoendelea na masomo)
na matokeo yake kuwasilishwa Bodi ya Mikopo na chuo chake.
7. Awe amemaliza Kidato cha Sita au awe na sifa linganishi (kama Diploma
n.k) ndani ya miaka mitatu (2015/2016 – 2017/2018).
8. Awe na umri usiozidi miaka 30 wakati wa kufanya maombi.
9. Waombaji ambao wazazi wao ni Wakurugenzi au Mameneja Waandamizi
katika Makampuni binafsi yanayotambuliwa na Mamlaka za Mapato na
Usajili hawatarajiwi kuomba;
10.Waombaji ambao wazazi wao ni viongozi wa umma au kisiasa ambao
wanatajwa na Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma hawatarajiwi
kuomba mikopo.
Mwisho wa kuomba mkopo in Septemba 4, 2017

Imetolewa na Bodi ya mikopo Kwa wanafunzi wa elimu ya juu nchini
HESLB

No comments:

Post a Comment